缅北禁地

Tabaka la Kati linalokua na mbadala wa uagizaji bidhaa toka nje Kutafungua mlango wa bidhaa zinazotengenezwa Afrika

Ethiopia's National Cement Plant in Dire Dawa, 15 March 2013. ? Gavin Houtheusen/Idara ya Maendeleo ya Kimataifa, kutoka Wikimedia.org

 

Mwandishi : Cristina Duarte, Msaidizi wa Katibu Mkuu na Mshauri wa Umoja wa Mataifa kuhusu Afrika

17 Novemba 2023

Kichwa cha makala hii kimetokana na mada ndogo ya kwanza ya msururu wa mazungumzo kuhusu Afrika 2023 ya Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Mshauri Maalumu kuhusu Afrika.

Tamko la kisera lilioandikwa na Ofisi ya Mshauri Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Afrika mwezi Mei 2023 liliaangazia takwimu zinazoonyesha kwamba idadi ya watu wa tabaka la kati barani Afrika inaweza kuongezeka hadi zaidi ya asilimia 40 ya jumla ya watu wote wote barani humo ifikapo 2060. 

Mabadiliko ya idadi ya watu yanaipatia Afrika fursa isiyo na kifani ya kuharakisha ukuaji wake wa viwanda, na kutoa mwanya wa Mapinduzi ya Nne ya Viwanda.

Mageuzi ya mazingira ya viwanda barani Afrika ni simulizi inayoingiliana kwa kina na kukua kwa tabaka la kati na mabadiliko ya kimkakati kuelekea mbadala wa uagizaji wa bidhaa za bara hili. 

Mahitaji na matakwa ya tabaka hili la kati linalostawi yana jukumu muhimu katika kuunda mwelekeo wa uchumi wa bara hili, ikiwa ni pamoja na Afrika kuchukua nafasi yake ipasavyo katika hatua ya uchumi wa dunia. Je, mienendo hii inaungana vipi ili kuathiri mpito wa Afrika kwa muundo wa viwanda  wa 4.0?

Tathimini ya jaribio la kihistoria la Afrika la mikakati ya mbadala wa bidhaa kutoka nje

Nchi za Kiafrika zilifuata mikakati ya uagizaji bidhaa kutoka miaka ya 1940 hadi 1950 na kutoka miaka ya 1960 hadi 1970. 

Hata hivyo, mikakati hii haikuzaa matunda. Katika miaka ya 1940 na 1950, serikali za kikoloni hazikuzingatia uanzishwaji wa viwanda kuwa kipaumbele cha sera, zikiona makoloni ya Kiafrika kama vyanzo tu vya malighafi ya bei ya chini na masoko ya kusafirisha bidhaa za viwandani. 

Katika miaka ya 1960, mundo ambao Mataifa yaliurithi kutoka kwa  wakoloni haukufaa kutoa mchakato endelevu wa maendeleo ya viwanda kwa kuzingatia mikakati ya uingizwaji wa bidhaa kutoka nje, hivyo nchi zinazotegemea bidhaa ziliibuka, zilizojengwa kwa misingi ya uchimbaji wa rasilimali.

Ripoti ya mwaka 2022 ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu kukuza amani ya kudumu na Maendeleo Endelevu barani Afrika inaangazia zaidi jambo hili. 

Nchi za Kiafrika zilipopata uhuru, zilirithi miundo ya utawala ambayo haikuundwa kuendesha Mataifa madhubuti yaliyojengwa juu ya maono ya mhusika aliye huru na mwenye uwezo, na sera jumuishi ya maendeleo ya viwanda.

Kiuchumi, wakati tawala za kikoloni zilizingatia uchimbaji wa rasilimali na ukusanyaji wa kodi, hazikukuza maendeleo ya kiuchumi, uzalishaji na uwekezaji. Pia zilitanguliza umuhimu wa kutumia mamlaka dhidi ya kuzingatia haki za watu binafsi kwa mujibu wa utawala wa sheria. 

Hata kuhusu matumizi ya ardhi, tawala hizi zililenga kudhibiti maeneo ya kimkakati kwa eneo lao au thamani ya kiuchumi badala ya kuhakikisha uwepo wa Serikali.

Wakati kuongeza uwezo wa matumizi ni mwanzo mzuri kwa muda mrefu, nchi za Afrika zinapaswa kubadilisha uchumi wake, zikilenga kuzalisha kwa ajili ya soko la ndani na nje ya nchi.

Kwa miongo mitano iliyopita, Afrika haijaweza kuepuka mtindo huu wa biashara wa enzi za ukoloni. Na utegemezi wa bara hilo kwa bidhaa kutoka nje umeunganisha uchumi wake kwa viwango vya chini kabisa vya minyororo ya thamani ya kimataifa. 

Kwa sababu ya miundo hii ya utegemezi wa bidhaa, bidhaa nyingi za ongezeko la thamani ambazo zinapendwa barani Afrika zinapatikana nje. Kadiri tabaka la kati linavyopanuka, ndivyo pia na hamu ya uagizaji wa bidhaa hizi zilizoongezwa thamani.

Kwa hivyo ni muhimu kujifunza masomo haya kutoka kwa historia ya bara la Afrika na majaribio yasiyofanikiwa ya kutekeleza mikakati ya uingizwaji wa bidhaa kutoka nje, na kuchukua mbinu ambayo inasimamia na kulinda maadili ya "Bidhaa zilizotengenezwa Afrika". 

Katika karne ya ishirini na moja, hali pia ni tofauti kabisa kwa sababu Afrika inaonyesha viwango vya juu vya utashi wa kisiasa kudhibiti mtiririko wake wa kiuchumi na kifedha.

Tabaka la kati la Afrika: Injini mpya ya ukuaji

Mwingiliano kati ya tabaka la kati linalokua la Afrika, biashara ya ndani ya Afrika na ukuaji wa viwanda unaweza kutumiwa ili kukuza ustawi wa kiuchumi wa Afrika. 

Kwa upande mmoja, kuongezeka kwa mahitaji ya bidhaa za matumizi ya ongezeko la thamani kunaweza kuimarisha mtiririko wa biashara ya ndani ya Afrika na kukuza uwezo wa uzalishaji. 

Hili pia linahitaji utekelezaji wa hatua madhubuti ili kuongeza ufanisi na ushindani wa uwezo huu huku ikipunguza hatari ya kuzidisha pengo la usawa lililopo katika biashara ya kimataifa ambalo kwa muda mrefu limekuwa likikwamisha uchumi wa Afrika.

Waafrika wote wanafahamu kwamba bara lazima lielekee kwenye mseto wa kiuchumi na mauzo ya nje ili kuwa tegemezi kidogo wa bidhaa na kupanda viwango vya minyororo ya thamani ya kimataifa. 

Lakini Waafrika pia wanapaswa kuelewa kwamba mikakati ya uingizwaji wa bidhaa barani Afrika inaweza kuharakisha juhudi hii kwa kufungua ukuaji wa viwanda barani humo, kuongeza uwezo wake wa kujenga kwa haraka utamaduni unaohitajika wa viwanda, kuunda nafasi za ajira zenye staha, kupanua wigo wa biashara na kuleta mseto wa uchumi, kuunganisha sekta binafsi na kuboresha kimataifa hifadhi ya usimamizi kuelekea kudumisha amani na utulivu wa kudumu.

Sambamba na simulizi ya “Kuibuka kwa Afrika” na kuongeza uwezo wa tabaka la kati linalokua barani Afrika sehemu ambayo inabakia kukabiliwa na mshtuko kutoka nje, ikiwa ni pamoja na wale wanaoishi kwa dola 2 hadi 4 kwa siku, bara hili linahitaji kujenga mzalishaji mpana zaidi wa uchumi, kuongeza uwezo wa manunuzi na kuwezesha mahitaji ya ufanisi katika sekta ya umma na binafsi. 

Wakati kuongeza nguvu ya matumizi ni mwanzo mzuri, kwa ajili ya muda mrefu, nchi za Afrika zinapaswa kubadilisha uchumi wake, zikilenga kuzalisha kwa ajili ya soko la ndani na nje ya nchi.