Ãå±±½ûµØ

Kwa nini COP27 ni muhimu kwa Sierra Leone

Get monthly
e-newsletter

Kwa nini COP27 ni muhimu kwa Sierra Leone

Ni matumaini yetu kwamba itasaidia kufuatilia kwa haraka mifumo ya ufadhili wa mabadiliko ya hali ya hewa na kuongeza kasi ya miradi inayoendelea ya kukabiliana na hali ya hewa.
Afrika Upya: 
4 Novemba 2022
The effect of deforestation on the hills  of Tombo, a coastal fishing town outside of the capital of
The effect of deforestation on the hills of Tombo, a coastal fishing town outside of the capital of Freetown in Sierra Leone

Sierra Leone ni miongoni mwa asilimia 10 ya nchi duniani ambazo ziko hatarini zaidi na athari kali za mabadiliko ya hali ya hewa, na kwa sasa ni mojawapo ya nchi zilizo na uwezo mdogo wa kukabiliana na athari hizo.

Ruwaza isiyotabirika ya hali ya hewa, mafuriko makubwa, maporomoko ya udongo, na uharibifu wa mazao unaohusishwa unazidi kuwa mara kwa mara, huku nchi ikishuhudia miti ikikatwa kwa kasi zaidi kuliko inavyopandwa.

Wanasayansi wa hali ya hewa wanatuambia kwamba ikiwa ulimwengu hautafikia kushuka kwa kasi kwa ongezeko la joto duniani katika miaka minane ijayo, majanga ya kiasili tuliyoshuhudia katika siku za hivi karibuni duniani kote yatakuwa mchezo wa watoto ikilinganishwa na yajayo.

COP27, Kongamano la 27 la Nchi Wanachama linaloendelea mjini Sharm El Sheikh, Misri, ni kongamano la kila mwaka la Umoja wa Mataifa la serikali, wanasayansi, na wadau wengine wakuu kutoka kote ulimwenguni kukagua maendeleo katika juhudi za kuepusha janga la mazingira, dhidi ya ahadi zilizomo katika mikataba ya kimataifa ya hatua za hali ya hewa.Ìý

Afrika, kanda ya kimataifa ambayo imechangia kwa uchache zaidi katika janga la mabadiliko la hali ya hewa linaoendelea, imepata hasara kubwa zaidi na uharibifu unaotokana na mabadiliko ya hali ya hewa yanayosababishwa na binadamu. Kwa hivyo, bara hili likiwa mwenyeji wa COP ya mwaka huu, jambo kuu litakuwa likitoa mwelekeo wa utekelezaji wa ahadi ambazo hazijatekelezwa kutoka kwa COP zilizopita.

Hii ni hasa kuhusiana na ahadi za kifedha zinazosubiri kutolewa na nchi tajiri kusaidia nchi zinazoendelea kama Sierra Leone ili kupunguza athari na kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Hoja lazima itolewe kwamba suala la kutimiza majukumu ya ufadhili wa mabadiliko ya hali ya hewa ya nchi zenye mapato ya juu kwa nchi zinazoendelea sio suala la utegemezi wa misaada bali la haki ya mabadiliko ya hali ya hewa.

Ìý

Lazima kuwe na mabadiliko katika mtazamo wa sera kuelekea mtazamo jumuishi ambao unashughulikia kwa wakati mmoja masuala mawili au zaidi yanayohusiana na maisha, uzalishaji wa ajira, maendeleo ya mtaji wa watu, afya ya umma, ulinzi wa mazingira, usawa wa kijinsia, usalama wa chakula, na upatikanaji wa nishati.

Kutakuwa na msukumo mkubwa wa kuongezeka kwa ufadhili kwa ajili ya ukabilifu na miradi ya kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa katika nchi za mapato ya chini na ya kati ili kuleta matokeo mema kwenye ukuaji wa uchumi, maendeleo ya kijamii na kuimarishwa kwa ustahimilivu dhidi ya mabadiliko ya hali ya hewa.Ìý

  • Mahitaji mahususi yatakuwa kwa nchi tajiri kutimiza ahadi zao za kila mwaka za dola bilioni 100 za ufadhili wa mabadiliko ya hali ya hewa na kuhusu kuongezeka maradufu kwa msaada wa kukabiliana na hali hewa hadi dola bilioni 40 ifikapo 2025 kama ilivyokubaliwa Glasgow mwaka jana wakati wa COP26.
  • Miongoni mwa mapendekezo mengine madhubuti yatakayojadiliwa kwa dhati katika COP27 ni kuanzishwa na kuwezesha ndani ya miaka mitano ijayo ya mfumo wa tahadhari ya mapema kwa dharura wa mabadiliko ya hali ya hewa ambao ungekumba dunia nzima.
  • Nyingine ni mpango wa miradi kamili kuhusu mabadilio ya hali ya hewa (karibu 400) katika maeneo kama vile kilimo, nishati, uchukuzi, teknolojia ya kidijitali na majukwaa, na bidhaa asilia.
  • Pia kutakuwa na umakini mkubwa kwa maamuzi na hatua, haswa ufadhili, kushughulikia 'hasara na uharibifu' ambao umezidi uwezo wa nchi kukabiliana nao.

Sierra Leone, kama nchi nyingi zinazoendelea, leo hii inakabiliwa na majanga mengi ya uhaba wa chakula, mzigo wa madeni, kupanda kwa gharama ya maisha, na upungufu wa nishati yanayoweza kupunguza umakinifu kwa hatari ya wazi na ya sasa inayoletwa na janga la mabadiliko ya hali ya hewa kwa ubinadamu.

Hoja lazima itolewe kwamba suala la kutimiza majukumu ya ufadhili wa mabadiliko ya hali ya hewa ya nchi zenye mapato ya juu kwa nchi zinazoendelea sio suala la utegemezi wa misaada bali la haki ya mabadiliko ya hali ya hewa.

Lakini, kutokana na kwamba changamoto zilizopo haziwezi kushughulikiwa kwa kutumia fedha za maendeleo zilizopo sasa na njia ya kawaida ya kufanya mambo, sasa ni wakati wa nchi kutumia vyema fursa ili kunufaika na ubunifu wa fedha za mabadiliko ya hali hewa na suluhisho endelevu.Ìý

Lazima kuwe na mabadiliko katika mtazamo wa sera kuelekea mtazamo jumuishi ambao unashughulikia kwa wakati mmoja masuala mawili au zaidi yanayohusiana na maisha, uzalishaji wa ajira, maendeleo ya mtaji wa watu, afya ya umma, ulinzi wa mazingira, usawa wa kijinsia, usalama wa chakula, na upatikanaji wa nishati.

Mfano mmoja rahisi ni mikakati ya nishati ya jua ambayo inahusiana moja kwa moja na uboreshaji wa shughuli za usindikaji wa mazao ya kilimo, vyanzo vya maji ya kunywa, utoaji wa huduma za afya, na muunganisho wa Mtandao kwa shule za sekondari katika wilaya zinazolengwa.

Mifano ya ubunifu zaidi na yenye matarajio mema ya suluhisho jumuishi ya maendeleo endelevu yataangaziwa, kujadiliwa na kuendelezwa kwenye COP27.

Ili kuimarisha ushiriki wa wajumbe wa ngazi ya juu kutoka Sierra Leone katika COP27, Serikali ya Sierra Leone ilijiunga na Umoja wa Mataifa, Ubalozi wa Uingereza, ujumbe wa Umoja wa Ulaya na wadau wengine kutoka katika jamii kwa Mazungumzo ya Hatua za Hali ya Hewa mwezi Oktoba 2022.

Kongamano hilo lilizingatia njia madhubuti ambazo Sierra Leone inaweza kutumia mali yake ya kiasili ya kuvutia (misitu, mali ya kilimo, rasilimali za maji, bioanuwai, na majaliwa ya jua) ili kupata fedha muhimu za mabadiliko ya hali ya hewa na suluhisho za asili kwa ajili ya kufufua uchumi wake na maendeleo ya muda mrefu.

So, as the continent hosts this year’s COP, the key preoccupation will be generating a roadmap for the implementation of unfulfilled promises from previous COPs. This is especially in relation to the pending financial pledges made by rich countries to support developing countries like Sierra Leone to lessen the impact of and adapt to climate change.

Ilikuwa wazi kutokana na mazungumzo hayo kwamba maliasili nyingi za Sierra Leone zingeweza kutumika vyema zaidi kuimarisha fedha na teknolojia ambazo nchi hiyo inahitaji kwa ukuaji wa uchumi jumuishi, wa kijani kibichi na endelevu, badala ya kuuza nje tu rasilimali muhimu kwa bei nafuu kama bidhaa za msingi.Ìý

Ni matumaini yetu kuwa ushiriki wa Sierra Leone katika COP27 utasaidia kuharakisha utekelezaji wa hatua muhimu zinazofuata zilizokubaliwa katika mazungumzo yanayohusiana na vielelezo vya ufadhili wa mabadiliko ya hali ya hewa na kuchochea kasi ya kuongeza kasi ya miradi inayoendelea ya kukabiliana na hali ya hewa nchini kote katika uhifadhi wa misitu, uzalishaji na usambazaji wa nishati ya jua na maji, uvuvi na usimamizi wa ufuo, na kilimo na usindikaji wa mazao ya kilimo. Inapasa pia kuimarisha dhamira ya kutimiza ahadi ambayo nchi imetoa kukomesha ukataji miti ifikapo 2030.Ìý

Kama ilivyo kwa ulimwengu wote, mabadiliko ya hali ya hewa yanaathiri kila nyanja ya uchumi na jamii ya Sierra Leone. COP27 kwa hiyo pia itatumika kusisitiza kwa kila mtu ukweli kwamba hatua za dharura za mabadiliko ya hali ya hewa si jukumu la serikali pekee.Ìý

Kwa hivyo, tunawahimiza wajumbe wa COP27, sio tu wa serikali, lakini pia kutoka kwa asasi za kiraia, sekta binafsi, vyombo vya habari, mashirika ya kimataifa ya maendeleo na taasisi za elimu ya juu, kurejea nchini kwa dhamira mpya na nia ya kuungana na kufuata hatua za dharura za mabadiliko ya hali ya hewa na kujihusisha kikamilifu na ufadhili wa hali ya hewa.Ìý

Ni kwa njia hii tu, nchi inaweza kushughulikia kikweli janga la mabadiliko ya hali ya hewa kwa namna ambayo inalinda rasilimali za kitaifa za mazingira, kujenga uwezo wa kustahimili majanga yanayohusiana na hali ya hewa, na kuendeleza maendeleo endelevu ambayo hayamwachi mtu nyuma.Ìý


Bw. Babatunde ÌýAhonsini Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Sierra Leone.

More from this author